P&L

P&L

Niyonzima kufanyiwa upasuaji India



Kiungo wa Simba Haruna Niyonzima anatarajia kwenda nchini India kufanyiwa upasuaji mdogo kwenye mguu unaomsumbua na kumfanya asionekane uwanjani siku za karibuni kutokana na kuuguza majeraha.
Afisa habari wa Simba Haji Manara wakati akizungumza na waandishi wa habari amesema, Niyonzima ataondoka nchini ndani ya siku mbili hizi kuelekea India kwa ajili ya matibabu.
“Haruna Niyonzima anatarajia kusafiri ndani ya siku hizi mbili kwenda India kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji mdogo kwenye mguu kutokana na maumivu yanayoendelea kumsumbua, haitachukua zaidi ya wiki mbili atakuwa amerejea uwanjani kwa sababu ni upasuaji mdogo tu”-Haji Manara, afisa habari Simba.
Niyonzima ambaye alisajiwa na Simba baada ya kumaliza mkataba wake na Yanga hajaonekana uwanjani katika mechi kadhaa na imekua ikielezwa kwamba ni kutokana na majeraha.

No comments